Monday, February 15, 2010

Seyyid Khalifa bin Harub


Jina lake hasa ni Syd Khalifa bin Harub bin Thuwein bin Said bin Sultan bin Imam Ahmed bin Said bin Mohammed bin Ahmed bin Khelef bin Said Al Azdy.
Kama kisambare Syd Khalifa alizaliwa akiwa kapiga rangi ya ubulu, kitu kilowatisha wakunga na watu wazima waliokuweko,  na wakanza kunong’ona, labda alijizonga na kitovu, labda kapata kisonge, labda subian labda labda labda, lakini kila siku kupita alirudisha ile rangi yake ya Kiafrika kama ya wazee wake. 


Ingawa alizaliwa Oman siku ya tarehe 26 mwezi wa Agosti mwaka 1879, mama yake toka hapo afya yake ikawa mbaya na yeye akafa na akawachwa Khalifa ni yatima, wa baba na mama. Ikabidi aondolewe kwao apelekwe kulelewa kwenye kasri ya Sultan Syd Feisal bin Turki, ambae ndie mjomba wake nae ndie Sultan wa Muskat.
Na Bwana huyu kufikia umri wa miaka 13 alilazimika kuja Unguja aje aitikie wito wa ami yake Syd Hemed bin Thuwein, aliyekuwa mfalme wa Zanzibar wakati huo, aliyetawala mwaka 1893 mpaka mwaka 1896
Kwa hivyo yeye ni mjukuu khalisi wa Syd Thuwein, aliyetawala Oman, ambae Mwenyezi Mungu Alimtunukia watoto wengi , akiwemo Syd Harub na Syd
Hemed. Na Syd Harub alikufa akiwa kijana sana. Mama yake aliitwa Turkiya binti Syd Turky bin Said Sultan, Syd Turky ni mtoto wa 5 wa Syd Sutan, ambae aliwahi kutawala Oman mwaka 1871 na akafa 1888, ambae ndie aliyemza huyo mama yake Syd Khalifa, na akaolewa na Syd Harub na akazaliwa yeye syd Khalifa.
Baada ya kufa baba yake Syd Khalifa alilelewa na babu yake Syd Turky na alilelewa pamoja na mjukuu mwengine wa Syd Turky yaani Syd Taimur na walilelewa kishujaa na mafunzo kede kede mpaka akapikika na alipokuja huku Zanzibar akazidi kuwa mahiri na mtaalam wa mengi, hasa  farasi.Siku aliyokuja hakuna
mtu yoyote aliyejuwa aliingia ghafla katika mwaka 1903, na meli aliokuja nayo ikiitwa Aboukir kabla ya kuja Zanzibar alipitia Makka kwa ajili ya ibada ya Umra, mara ya pili alikwenda na shemeji yake Syd  Ali , na huko ndiko alipokutana na mkewe bi Matuka na wakapendana, ambae naye yeye alifuatana na harimu yake, kaka Ali bin Humud ambae nae pia aliwahi kuwa Sultan wa Zanzibar 
Syd Khalifa aligota milango mingi ikiwemo hata ya mambo ya michezo kama ya sailing, polo, tennis na milango kadha wakadha ya kidunia na ya kiakhera [Dini] alimradi  aliishi. Alihudhuria mabaraza mengi sana akiwa 
bado mtoto, kitu kilompelekea kuwa kiongozi mzuri baadae, na kumudu kukaa kwenye kiti cha usultani kwa muda mrefu zaidi. Aliowa alipotawala Syd Humud Baada ya kufa Syd Hemed, alimuowa yule yule mpenzi wake Sayyidah Matuka binti Humud, mtoto wa Syd Humud aliyezaa na mkewe Seyyidah Khoufara binti Majid bin Sutan.


Syd Khalifa alipata watoto wawili, baada ya kufa mmoja alizaliwa Syd Prince Sir Abdalla 12 feb 1910. na alipokufa Bi Matuka Ndipo alipomuowa Bi Nunuu binti Ahmed. Alitawala tarehe 9 Disember mwaka 1911 , na yeye ni miaka 32, ingawa kiti hicho ilikuwa atawale Syd Khalid bin Muhammed, 
lakini Bwana huyu alikataa kata kata kutawala na akajitia maradhi.Alitawala kwa miaka 49  ni miaka mingi, kuliko Sultani yoyote wazanzibar, alimaliza mwaka 1960.
Na moja ya kazi yake kubwa alitufunguwa uso Wazanzibari kwa kuwasaidia Waingereza katika vita viwili vikuu.
 Syd Khalifa alifariki Dunia saa 9 alfajiri ya Jumapili ya tarehe 9 October mwaka 1960, sawa sawa na Mwezi 17 Rabil Thani 1380 Hijra. na kuwacha majonzi makubwa sehemu kubwa ya Dunia si Ulaya, si Bara hindi si Afrika wala Uarabuni kila alomfahamu alijuwa kuwa Zanzibar imeondokewa, kwani alikuwa ni mtu wa watu sana.

No comments:

Post a Comment